Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa,
anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu:
Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu,
ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu.
Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu
na kuwapa nguvu wenye majuto.
Maana sitaendelea kugombana
wala kuwakasirikia siku zote,
maana hao niliowaumba watazimia mbele yangu,
nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uzima.