1
Isaya 53:5
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Lakini aliumizwa kwa sababu ya zambi zetu, alipondwa kwa sababu ya maovu yetu. Kwa kuazibiwa kwake sisi tumepata uzima; kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
Compare
Explore Isaya 53:5
2
Isaya 53:6
Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.
Explore Isaya 53:6
3
Isaya 53:4
Hata hivyo alitwaa mateso yetu, na kubeba huzuni zetu. Sisi tulifikiri amepata azabu, amepigwa na Mungu na kuteswa.
Explore Isaya 53:4
4
Isaya 53:3
Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.
Explore Isaya 53:3
5
Isaya 53:7
Alionewa na kuteswa, lakini alivumilia kwa unyenyekevu, bila kutoa sauti hata kidogo. Alikuwa kama mwana-kondoo anayepelekwa kwenda kuchinjwa, kama kondoo anavyokaa kimya anapokatwa manyoya. Hakutoa sauti hata kidogo.
Explore Isaya 53:7
6
Isaya 53:10
Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.
Explore Isaya 53:10
7
Isaya 53:2
Maana, mbele ya Yawe, mutumishi wake alikomaa kama kichipukizi, kama muzizi katika inchi kavu. Hakukuwa na umbo wala sura ya kupendeza, wala hakukuwa na uzuri wowote wa kutuvuta.
Explore Isaya 53:2
8
Isaya 53:12
Kwa hiyo nitamugawanyia sehemu pamoja na wakubwa, atagawanya vitu vilivyotekwa pamoja na wenye nguvu. Alijitoa yeye mwenyewe hata kufa; aliwekwa kundi moja na watu wakosaji. Alizibeba zambi za watu wengi, akawaombea musamaha hao wakosaji.
Explore Isaya 53:12
9
Isaya 53:11
Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.
Explore Isaya 53:11
10
Isaya 53:8
Alikamatwa kwa kinguvu, akahukumiwa na kupelekwa kuuawa; na hakuna mutu aliyejali mambo yanayomupata. Alifukuzwa kutoka inchi ya wanaokuwa wazima, kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
Explore Isaya 53:8
11
Isaya 53:9
Walimuzika pamoja na waovu; katika kifo aliwekwa pamoja na watajiri, ingawa hakutesa watu hata kidogo, wala hakusema neno lolote la udanganyifu.
Explore Isaya 53:9