Wengi waliomwona walishituka,
kwa vile sura yake ilikuwa imeharibika;
hakukuwa tena na umbo la mwanadamu!
Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi.
Wafalme watapumbazika kwa sababu yake,
maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa,
na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.