Kisha, Yawe akanijibu hivi:
Uyaandike maono haya;
uyaandike wazi juu ya vibao,
anayepitia pale apate kuyasoma haraka.
Maono haya yanangoja wakati uliopangwa;
ni maono ya ukweli juu ya mwisho.
Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee;
hakika yatafika, wala hayatachelewa.