Lakini upinde wake bado imara,
na mikono yake imepewa nguvu,
kwa uwezo wa Mwenye Nguvu wa Yakobo,
kwa jina la Muchungaji, Mulinzi wa Israeli.
Mungu wa baba yako atakusaidia,
Mungu Mwenye Nguvu atakubariki,
upate baraka za mvua toka juu mbinguni,
baraka za maji ya vilindi vinavyokuwa chini,
baraka za uzazi wa wamama na nyama.