Kisha Israeli akamubariki Yosefu, akisema:
“Mungu ambaye babu zangu
Abrahamu na Isaka walimutii katika maisha yao,
Mungu ambaye ameniongoza katika maisha yangu mpaka leo,
na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote,
awabariki vijana hawa!
Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka,
yadumishwe katika vijana hawa;
nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”