1
Muhubiri 7:9
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Usikuwe mwepesi wa hasira, maana, hasira inakaa ndani ya wapumbafu.
Compare
Explore Muhubiri 7:9
2
Muhubiri 7:14
Katika siku za kufanikiwa ukuwe na furaha. Katika siku za hasara ufikiri juu ya jambo hili: Mungu amefanya hiyo ya kwanza iambatane na ya pili kusudi mwanadamu asipate kujua mambo yatakayotukia nyuma yake.
Explore Muhubiri 7:14
3
Muhubiri 7:8
Mwisho wa jambo ni afazali kuliko mwanzo wake. Moyo muvumilivu ni bora kuliko moyo wa majivuno.
Explore Muhubiri 7:8
4
Muhubiri 7:20
Hakika, hakuna mutu wa haki katika dunia anayetenda vizuri siku zote bila kutenda zambi.
Explore Muhubiri 7:20
5
Muhubiri 7:12
Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.
Explore Muhubiri 7:12
6
Muhubiri 7:1
Sifa nzuri ni bora kuliko marasi ya bei kali. Siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa.
Explore Muhubiri 7:1
7
Muhubiri 7:5
Afazali kusikia maonyo ya wenye hekima kuliko kusikiliza nyimbo za wapumbafu.
Explore Muhubiri 7:5
8
Muhubiri 7:2
Afazali kwenda kwenye kilio, kuliko kwenda kwenye karamu, kwa sababu inawapasa wenye kuwa wazima kukumbuka kwamba kifo kinawangojea sisi wote.
Explore Muhubiri 7:2
9
Muhubiri 7:4
Moyo wa mwenye hekima uko ndani ya nyumba ya kilio, lakini moyo wa mupumbafu unapenda raha.
Explore Muhubiri 7:4