1
Wakolosayi 2:6-7
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Basi kwa sababu mumemukubali Kristo kuwa Bwana wenu, muishi katika kuungana naye. Mukuwe na mizizi ndani yake, mujijenge juu yake na kusimama imara katika imani sawa vile mulivyofundishwa. Na zaidi ya hii mukuwe wenye kushukuru sana.
Compare
Explore Wakolosayi 2:6-7
2
Wakolosayi 2:8
Mujiangalie hata mutu asiwapotoshe kwa elimu yake ya udanganyifu mutupu inayotegemea desturi za watu na roho mbaya zinazotawala dunia, lakini haitegemei mafundisho ya Kristo.
Explore Wakolosayi 2:8
3
Wakolosayi 2:13-14
Zamani mulikuwa mumekufa kwa sababu ya zambi zenu na kwa sababu mulikuwa watu wa mataifa mengine, wasiotahiriwa. Lakini sasa, Mungu amewapatia ninyi uzima pamoja na Kristo, naye ametusamehe zambi zetu zote. Alifuta barua ya madeni yetu na sherti zilizotushitaki. Aliyafuta kabisa kwa kuyapigilia juu ya musalaba.
Explore Wakolosayi 2:13-14
4
Wakolosayi 2:9-10
Kwa maana ukamilifu wote wa Mungu uko ndani ya Kristo katika mwili wake. Na kwa kuungana naye, ninyi mumepata kukamilika. Yeye ndiye anayetawala roho zote zenye mamlaka na uwezo.
Explore Wakolosayi 2:9-10
5
Wakolosayi 2:16-17
Basi, mutu asiwahukumu juu ya chakula au kinywaji, au juu ya kushika sikukuu fulani, ikiwa sikukuu ya Mwandamo wa Mwezi au siku ya Sabato. Mambo hayo yote ni kivuli cha mambo yatakayokuja, lakini ukweli wa mambo yote ni Kristo mwenyewe.
Explore Wakolosayi 2:16-17
Home
Bible
Plans
Videos