Watumishi wa mufalme wakamwambia Akisi: “Huyu si Daudi, mufalme wa inchi ya Israeli? Si huyu ambaye walikuwa wakiimbiana juu yake katika ngoma, wakisema: ‘Saulo ameua maelfu yake na Daudi ameua elfu makumi yake?’ ”
Daudi akafikiri sana juu ya maneno yale, akaanza kumwogopa sana Akisi mufalme wa Gati.