Saulo alimwelezea mwana wake Yonatani na wakubwa wake juu ya mupango wake wa kumwua Daudi. Lakini Yonatani, mwana wa Saulo, alimupenda sana Daudi. Kwa hiyo, akamwambia: “Baba yangu anakusudia kukuua. Hivyo, ufanye angalisho. Kesho asubui, ujifiche pahali pa siri, ukae pale.