Vilevile walikuwa wanacheza na kuimba nyimbo za kuitikiana hivi:
“Saulo ameua maelfu yake,
na Daudi ameua elfu yake makumi.”
Saulo hakupendezwa na maneno ya wimbo huo. Akakasirika sana. Akasema: “Wamemupa Daudi elfu makumi, lakini mimi wamenipa maelfu tu. Linalobakia ni kumupa Daudi ufalme.”