1
1 Wakorinto 2:9
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Lakini ni kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kuyaona wala kuyasikia, mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kufikiri juu yake, ndiyo yale Mungu aliyowatayarishia wale wanaomupenda.”
Compare
Explore 1 Wakorinto 2:9
2
1 Wakorinto 2:14
Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.
Explore 1 Wakorinto 2:14
3
1 Wakorinto 2:10
Lakini Mungu ametufunulia sisi siri yake kwa njia ya Roho wake. Maana Roho anachunguza vitu vyote, hata mipango ya Mungu inayofichwa kabisa.
Explore 1 Wakorinto 2:10
4
1 Wakorinto 2:12
Na sisi hatukupokea roho ya dunia hii, lakini tulipokea Roho anayetoka kwa Mungu, kusudi tupate kujua vitu vyote tulivyojaliwa kwa neema ya Mungu.
Explore 1 Wakorinto 2:12
5
1 Wakorinto 2:4-5
Mafundisho yangu na mahubiri yangu hayakutolewa kwa maneno ya werevu na hekima ya kimutu, lakini katika onyesho la uwezo wa Roho wa Mungu, kusudi imani yenu isikuwe katika hekima ya watu, lakini katika uwezo wa Mungu.
Explore 1 Wakorinto 2:4-5
Home
Bible
Plans
Videos