1
1 Wakorinto 13:4-5
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Upendo unavumilia, ni wenye wema; upendo hauna wivu, upendo haujivuni, na hauna kiburi. Upendo haukosi kuwa na adabu, hautafuti faida yake mwenyewe, haukasiriki upesi, nao hauhesabii mutu ubaya.
Compare
Explore 1 Wakorinto 13:4-5
2
1 Wakorinto 13:7
Upendo hauchoki na mambo yote, unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote na kuvumilia mambo yote.
Explore 1 Wakorinto 13:7
3
1 Wakorinto 13:6
Upendo haufurahii ubaya, lakini unafurahia ukweli.
Explore 1 Wakorinto 13:6
4
1 Wakorinto 13:13
Basi sasa, hivi vitu vitatu vinadumu: imani, tumaini na upendo; lakini kinachokuwa kikubwa kuliko hivi vingine ni upendo.
Explore 1 Wakorinto 13:13
5
1 Wakorinto 13:8
Upendo haukomi hata kidogo. Lakini kutabiri kunatoweka, zawadi ya kusema kwa luga za ajabu inatoweka, na maarifa yanapita.
Explore 1 Wakorinto 13:8
6
1 Wakorinto 13:1
Hata nikiwa na uwezo wa kusema luga za watu na za wamalaika, lakini kama sina upendo, masemi yangu ni bure kama vile kelele la kengele au matoazi.
Explore 1 Wakorinto 13:1
7
1 Wakorinto 13:2
Hata nikiwa na zawadi ya kutabiri, na uwezo wa kujua mafumbo yote na maarifa yote; hata nikiwa na imani kubwa inayoweza kuhamisha milima; lakini kama sina upendo, mimi ni kitu bure.
Explore 1 Wakorinto 13:2
8
1 Wakorinto 13:3
Ninaweza vilevile kugawanya mali yangu yote kwa kulisha wamasikini na hata kutoa mwili wangu uunguzwe, lakini kama sina upendo, hakuna faida ninayopata.
Explore 1 Wakorinto 13:3
9
1 Wakorinto 13:11
Wakati nilipokuwa mutoto, nilisema kama mutoto, niliwaza kama mutoto, nilifikiri kama mutoto. Lakini nilipokuwa mutu muzima niliacha mambo ya kitoto.
Explore 1 Wakorinto 13:11
Home
Bible
Plans
Videos