Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021预览

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

30天中的第25天

Anayosema Elihu, je, ni maswali ya kumdharau Ayubu? Siyo kwamba Ayubu ameshajua hayo yote na kumwamini Mungu? Ndiyo. Hata hivyo tunahitaji kukumbushwa ukuu utishao wa Mungu ili tusifanane na wale walio na hekima mioyoni (m.24). Ni watu wanaotafuta hekima kwao wenyewe badala ya kuzifikiri kazi za Mungu za ajabu. Tufanye anavyoshauri Elihu katika m.14: Simama kimya, uzifikiri kazi za Mungu za ajabu. Sisi binadamu tunalo giza fulani katika kumfahamu Mwenyezi. Hatuwezi kumwona. Ndiyo maana mwishoni Elihu anakiri kuwa tunapaswa kunyenyekea mbele ya Mungu wakati wote.

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 1 Wakorintho na Ayubu. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu

More