Maelezo ya mpango
Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F33529%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Hakuna mtu aliyekuwa amemwomba Yesu amsaidie huyu mjane, maana hakuna mtu aliyetegemea kwamba Yesu ataweza kufanya mwujiza kama huu. Ni mara ya kwanza kwa Yesu kumfufua mfu. Alifanya hivyo kwa sababu alimwonea huruma huyo mjane ambaye maisha yake sasa yangekuwa magumu mno (m.13, Bwana alipomwona alimwonea huruma, akamwambia, Usilie). Badala ya kulia naye akasema Usilie. Badala ya kukaa mbali akakaribia na kuligusa geneza, tendo ambalo lilimnajisi kutokana na sheria za Wayahudi. Akasema neno tu akawa hai! Hofu ikawashika wote, wakamtukuza Mungu (m.16). Ukitaka kumtukuza Mungu vilevile, unaweza kutumia maneno ya Efe 3:20-21: Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; naam, atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina.
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F33529%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Oktoba pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma k...
More
http://www.somabiblia.or.tz