Soma Biblia Kila Siku 02/20Mfano

Yesu anasisitiza kwamba tusishangae ikiwa hali ya maisha yetu kama wafuasi itafanana na hali yake mwenyewe. Maana yeye ni mwalimu, sisi ni wanafunzi. Mwanafunzi hampiti mwalimu wake, wala mtumwa hampiti bwana wake. Yamtosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumwa kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mwenye nyumba Beelzebuli, je! Si zaidi wale walio wa nyumbani mwake? (m.24-25). Yesu anajua maneno haya yanaweza kututia hofu, kwa hiyo anasisitiza mara tatu: Msiogope(m.26, 28, 31). Hata kama watu watajaribu kutulazimisha kulikana jina lake, tusiogope, maana yeye atakuwa pamoja nasi papo hapo na kututia nguvu. Na hata tukiuawa tutashinda tu, maana ajuaye yote na mwenye kuhukumu yuko upande wetu, ni Baba yetu!
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 02/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Mathayo na Esta. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12/2020

MWANGA Kuvutiwa Maishani Na Mwanga Ajabu Wa Mungu

Soma Biblia Kila Siku 10/2020

Soma Biblia Kila Siku 07/2020

Kuwa Karibu Na Mungu Kila Siku

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Moyo - Neno La Mungu Hugeuza Moyo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Upendo Wa Bure
