Soma Biblia Kila Siku 02/20Mfano

Ni vema kufurahi na kupelekeana zawadi tukitokewa na jambo jema kibinafsi au kitaifa. Huzuni aliyokusudia Hamani kwa Wayahudi iligeuzwa kuwa shangwe kutokana na maombi ya Esta kwa mfalme na kuingilia kwa Mungu. Iliamuriwa kusherehekea siku hiyo kila mwaka na kuwakumbuka maskini. Hata leo kuna sikukuu ya Purimu huko Israeli (puri = kupiga kura; kama ilivyoelezwa katika 3:7, Mwezi wa kwanza, ndio mwezi wa Nisani, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani). Linganisha na Pasaka na Krismasi, watu wakipeleka zawadi kwa wagonjwa n.k. Wewe unasherekeaje siku kuu zako na za nchi? Mungu anapewa sehemu gani?
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 02/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Mathayo na Esta. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12/2020

MWANGA Kuvutiwa Maishani Na Mwanga Ajabu Wa Mungu

Soma Biblia Kila Siku 10/2020

Soma Biblia Kila Siku 07/2020

Kuwa Karibu Na Mungu Kila Siku

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Moyo - Neno La Mungu Hugeuza Moyo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Upendo Wa Bure
