Soma Biblia Kila Siku 10Mfano

Kufanikiwa kuna hatari, nayo ni kiburi! Tazama m.6 ambapo Mwimba Zaburi anasema kama mpumbavu:Nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele(ling. Zab 10:6 ambapo mtu anasema vivyo hivyo:Sitaondoshwa, kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni). Kwa hiyo akapatwa na hasira ya Mungu, akataka kufa. Lakini akagundua kuwa hasira ya Mungu kwa watu wake ni ya kitambo, yaani, inadumu mpaka tuombe radhi kwake:Ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, katika radhi yake mna uhai(m.5). Je, unajua kuwa tunaishi kwa sababu Mungu anatulinda na kutuepusha na kifo? Au kwamba kama tukifanikiwa na kuinuliwa katika maisha, ni kwa sababu ya wema wa Mungu? Tumshukuru Mungu kwa mema mengi tupatayo maishani ili tusijivune na kufa!
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 10 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Warumi na 1 Samweli.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku 10/2020

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku 07/2020

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021
