Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 30:1-12

Zab 30:1-12 SUV

Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu. Ee BWANA, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya. Umeniinua nafsi yangu, Ee BWANA, kutoka kuzimu. Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni. Mwimbieni BWANA zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake. Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, Katika radhi yake mna uhai. Huenda kilio huja kukaa usiku, Lakini asubuhi huwa furaha. Nami nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele. BWANA, kwa radhi yako Wewe uliuimarisha mlima wangu. Uliuficha uso wako, Nami nikafadhaika. Ee BWANA, nalikulilia Wewe, Naam, kwa BWANA naliomba dua. Mna faida gani katika damu yangu Nishukapo shimoni? Mavumbi yatakusifu? Yataitangaza kweli yako? Ee BWANA, usikie, unirehemu, BWANA, uwe msaidizi wangu. Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha. Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. Ee BWANA, Mungu wangu, Nitakushukuru milele.

Soma Zab 30

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zab 30:1-12

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha