Soma Biblia Kila Siku 10Mfano

Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho (m.5). Hii ina maana ya kwamba ukitaka kuishinda dhambi katika maisha yako ya Kikristo kwa nguvu zako mwenyewe (waufuatao mwili), utakwama, na utabaki tu kutamani dhambi (huyafikiria mambo ya mwili). Lakiniukimtegemea Kristo na kuufikiria ukombozi aliokushindia (waifuatao roho), maisha yako yatakuwa na matunda mema (huyafikiri mambo ya roho). Zingatia kwa makini Yesu anayosema: Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote(Yn 15:5). Matunda hayo tunayozaa tunapokaa ndani ya Yesu, ni kazi ya Roho anayekaa ndani yetu. Kwa hiyo huitwa tuna la Roho: Tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria(Gal 5:22-23).
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 10 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Warumi na 1 Samweli.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku 10/2020

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku 07/2020

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021
