Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku 6Mfano

Soma Biblia Kila Siku 6

SIKU 23 YA 30

Sauti ya Mungu hutuita katika hali mbalimbali. Inatuita hata sasa kwa njia ya neno hili la leo. Lengo la Mungu ni kutushauri tuache ujinga, upumbavu na dharau. Kutoisikiliza sauti ya Mungu ndiko kunakosababisha kukosa utii kwake. Matokeo ya kutotii ni kutengwa na Mungu. Tunapohitaji msaada kwake hatatusikiliza. Hakuna kitu kichungu kuliko kuachwa na Mungu. Ukikosa Mungu, utapata wapi kimbilio? Mtii Mungu, na utakuwa na amani na mafanikio. Rudia m.23 ukizingatia maana yake katika maisha yako: Geukeni kwa ajili ya maonyo yangu; Tazama, nitawamwagia roho yangu, Na kuwajulisheni maneno yangu.

siku 22siku 24

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 6

Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.

Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha