Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku 6Mfano

Soma Biblia Kila Siku 6

SIKU 25 YA 30

Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe (m.28). Mtumishi wa Bwana hapa ajifunze: 1.Asifikirie kulitunza kundi tu lakini pia akumbuke kujitunza nafsi yake! 2.Kwa njia gani atunze kundi na nafsi yake? a) Alishe kwa neno la neema (m.28: Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe; m.32: Nawaweka katika mikono ya Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliotakaswa). b) Alinde(m.29-30 inatoa sababu: Mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi;tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao). c) Akeshe(m.31:kesheni, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana). d) Aonye(m.31: Sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi). e) Ajiweke mikononi mwa Mungu(m.32: Nawaweka katika mikono ya Mungu). f) Awasaidie wanyonge (m.35: Kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge). 3.Kanisa si lake Paulo (wala mtu mwingine yeyote), bali ni mali ya Yesu!

siku 24siku 26

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 6

Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.

Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha