Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Ishi Maisha -Yaliyojaa Kusudi!Mfano

Ishi Maisha -Yaliyojaa Kusudi!

SIKU 1 YA 7

“Sheria ya Dhahabu”


Iwe ni mwanasiasa, mfanyabiashara, mnenaji wa makongamano, au   hata mtu wa kawaida, watu kutoka kila aina ya maisha mara kadhaa hurejea wema   wa Sheria ya Dhahabu. Ukweli ni kwamba, kila mtu alishaisikia na anajua maana   yake.


Watu wengi watakubali kuwa “kuwafanyia wengine kama ambavyo   tungejifanyia sisi” ni jambo la muhimu katika jamii. Katika maeneo mengi, ni utaratibu unaobeba   utamaduni wa watu, familia na urafiki pamoja. Sheria ya Dhahabu inaonyesha sifa   ya kuwatumikia wengine, kuonyesha ukarimu na kuwasaidia wao walio katika  uhitaji. 


Yesu alikuwa  ni   mwanzilishi wa Sheria ya Dhahabu, ambayo ni moja ya vipaumbele muhimu vya   maisha ya Kikristo yaliyofanikiwa. 


Kama   Wakristo, Mungu amemuita kila mmoja wetu kuikuza imani yake katika kiwango   cha kuwa si watu wanaoamini juu ya Mungu tu. Shauku yake ni kila mmoja wetu   kuweka imani yake katika matendo kwa kugusa maisha ya wengine, kwamba   tumtukuze Mungu kwa kuonyesha upendo na neema Yake kwao.Hii ndio kuishi kwa   kweli kwa Sheria ya Dhahabu.

Andiko

siku 2

Kuhusu Mpango huu

Ishi Maisha -Yaliyojaa Kusudi!

Maisha yenye kusudi na yaliyojaa furaha, hujengwa kwenye mahusiano, upendo na imani. Kama unataka njia iliyonyooka zaidi ya mpango wa Mungu kwa maisha yako, tumia mpango huu kukusaidia kuweka mkazo katika hilo lengo lako...

More

Tungependa kuwashukuru Twenty20 Faith, Inc. kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.twenty20faith.org/yvdev2

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha