Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Injili Ulimwenguni - Sehemu 1Mfano

Injili Ulimwenguni - Sehemu 1

SIKU 4 YA 7

  

Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria, kwa mujibu wa Sheria ya Mose, Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana, (kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa, katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”

Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.Simeoni akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria, ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:

“Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi,sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,ulioweka tayari machoni pa watu wote,nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.” Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto. Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike na upanga utauchoma moyo wako.” Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke mzee sana, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana, naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa. Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.Wakati uo huo, Ana alikuja akaanza kusifu akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu. Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.A Naye mtoto Yesu akakua na kuongezeka nguvu akiwa amejaa hekima na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.

Andiko

siku 3siku 5

Kuhusu Mpango huu

Injili Ulimwenguni - Sehemu 1

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadi...

More

Tungependa kumshukuru GNPI Afrika kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: 
http://gnpi-africa.org/

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha