Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Somabiblia Kila Siku 3Mfano

Somabiblia Kila Siku 3

SIKU 8 YA 31

Mungu ndiye aliyewafanya Wayahudi wengi kuwa na mioyo migumu: Amewapofusha macho, Ameifanya mizito mioyo yao; Wasije wakaona kwa macho yao ...(m.40). Aliyotabiri nabii Isaya yakatimizwa. Na wale viongozi walioamini hawakukiri kwa wazi: Kwa maana walipenda utukufu wa wanadamu kuliko utukufu wa Mungu (m.42f). Lakini mtu anayetaka kuwa mfuasi wa Yesu kwa siri, yuko hatarini kupoteza imani yake (ling. Mt 10:32-33: Kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni. Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni). Je, kwako ni muhimu zaidi kupata sifa kwa nani?

Andiko

siku 7siku 9

Kuhusu Mpango huu

Somabiblia Kila Siku 3

SomaBiblia Kila Siku 3 ni mpango mzuri wa kukusaidia kusoma Biblia kwa njia rahisi. Ufafanuzi wa somo la kila siku unakupa mwanga na kiu ya kuendelea kulitafakari Neno la Mungu ukiwa peke yako au pamoja na wenzako.

Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha