Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Somabiblia Kila Siku 3Mfano

Somabiblia Kila Siku 3

SIKU 18 YA 31

Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe(m.11). Furaha ni jambo muhimu na la msingi katika Ukristo! Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini(Flp 4:4). Itakuwaje furaha ya Yesu kuwa ndani yetu? 1.Kwa kuutambua upendo wake kwetu na kuupokea (m.9 na 12-13). 2.Kwa kuzitii amri zake na kuzifuata (m.10). Ni amri kama hii: Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi(m.12 na 17). Tukishapokea upendo wake, yaani wokovu wake, twapata moyo mpya unaompenda Yesu na amri zake.

siku 17siku 19

Kuhusu Mpango huu

Somabiblia Kila Siku 3

SomaBiblia Kila Siku 3 ni mpango mzuri wa kukusaidia kusoma Biblia kwa njia rahisi. Ufafanuzi wa somo la kila siku unakupa mwanga na kiu ya kuendelea kulitafakari Neno la Mungu ukiwa peke yako au pamoja na wenzako.

Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha