Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 119:5-8 - Linganisha Matoleo Yote

Zaburi 119:5-8 BHN (Biblia Habari Njema)

Laiti mwenendo wangu ungeimarika, kwa kuyafuata masharti yako! Nikizingatia amri zako zote, hapo kweli sitaaibishwa. Nitakusifu kwa moyo mnyofu, nikijifunza maagizo yako maadilifu. Nitayafuata masharti yako; usiniache hata kidogo.

Shirikisha
Zaburi 119 BHN

Zaburi 119:5-8 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)

Ningependa njia zangu ziwe thabiti, Nizitii amri zako. Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote. Nitakushukuru kwa unyofu wa moyo, Nikiisha kujifunza hukumu za haki yako Nitazitii amri zako, Usiniache kabisa

Shirikisha
Zaburi 119 SUV

Zaburi 119:5-8 SRUV (Swahili Revised Union Version)

Ningependa njia zangu ziwe thabiti, Nizitii amri zako. Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote. Nitakushukuru kwa unyofu wa moyo, Nikiisha kujifunza hukumu za haki yako. Nitazitii amri zako, Usiniache kabisa.

Shirikisha
Zaburi 119 SRUV

Zaburi 119:5-8 NEN (Neno)

Laiti mwenendo wangu ungekuwa imara katika kuyatii maagizo yako! Hivyo mimi sitaaibishwa ninapozingatia amri zako zote. Nitakusifu kwa moyo mnyofu ninapojifunza sheria zako za haki. Nitayatii maagizo yako; usiniache kabisa.

Shirikisha
Zaburi 119 NEN