Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Methali 28:1-6

Methali 28:1-6 BHN

Waovu hukimbia japo hawafukuzwi na mtu, lakini waadilifu ni hodari kama simba. Taifa la fujo huzusha viongozi wengi, lakini kwa kiongozi mmoja mwenye akili na maarifa huwa na utengemano Mtu mhitaji anayewadhulumu maskini, amefanana na mvua kubwa inayoharibu mimea. Watu wanaovunja sheria huwasifu waovu, lakini wanaoishika sheria hupingana nao. Waovu hawajui maana ya haki, lakini wamchao Mwenyezi-Mungu wanaielewa kabisa. Afadhali maskini aishiye kwa unyofu, kuliko tajiri aishiye kwa upotovu.

Soma Methali 28