Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 75:1-10

Zaburi 75:1-10 SRUV

Ee Mungu, tunakushukuru. Tunakushukuru kwa kuwa Jina lako liko karibu; Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu. Nitakapoufikia wakati ulioamriwa, Mimi nitahukumu hukumu za haki. Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki, Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake. Niliwaambia waliojivuna, Msijivune; Na wasio haki, Msiiinue pembe. Msiiinue pembe yenu juu, Wala msinene kwa shingo ya kiburi. Maana siko mashariki wala magharibi, Wala nyikani itokako heshima. Bali Mungu ndiye ahukumuye; Humdhili huyu na kumwinua huyu. Maana mkononi mwa BWANA mna kikombe, Na mvinyo yake inatoka povu; Kumejaa machanganyiko; Naye huyamimina. Na sira zake wasio haki wa dunia Watazifyonza na kuzinywa. Bali mimi nitatangaza matendo yako milele, Nitamwimbia Mungu wa Yakobo. Nguvu zote za wasio haki nitazimaliza, Lakini nguvu za mwenye haki nitaziimarisha.

Soma Zaburi 75

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha