Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 75

75
Shukrani kwa wema aliotenda Mungu
Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Usiharibu. Zaburi ya Asafu. Wimbo.
1Ee Mungu, tunakushukuru.
Tunakushukuru kwa kuwa Jina lako liko karibu;
Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.
2Nitakapoufikia wakati ulioamriwa,
Mimi nitahukumu hukumu za haki.
3 # Ebr 1:3 Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki,
Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake.
4Niliwaambia waliojivuna, Msijivune;
Na wasio haki, Msiiinue pembe.
5Msiiinue pembe yenu juu,
Wala msinene kwa shingo ya kiburi.
6Maana siko mashariki wala magharibi,
Wala nyikani itokako heshima.
7 # 1 Sam 2:7; 2 Sam 5:2; Dan 2:21; Lk 1:52 Bali Mungu ndiye ahukumuye;
Humdhili huyu na kumwinua huyu.
8 # Ayu 21:20; Yer 25:15; Ufu 14:10 Maana mkononi mwa BWANA mna kikombe,
Na mvinyo yake inatoka povu;
Kumejaa machanganyiko;
Naye huyamimina.
Na sira zake wasio haki wa dunia
Watazifyonza na kuzinywa.
9Bali mimi nitatangaza matendo yako milele,
Nitamwimbia Mungu wa Yakobo.
10Nguvu zote za wasio haki nitazimaliza,
Lakini nguvu za mwenye haki nitaziimarisha.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 75: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha