Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 52:1-9

Zaburi 52:1-9 SRUV

Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote. Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila. Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli. Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila. Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai. Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka; Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa kimbilio lake. Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kufanya mali kimbilio lake. Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele. Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako.

Soma Zaburi 52