Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mithali 28:1-6

Mithali 28:1-6 SRUV

Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni wajasiri kama simba. Kwa sababu ya maasi ya nchi wakuu wake huwa wengi; Bali kwa wenye ufahamu na maarifa hali ya nchi hudumishwa Mtu mhitaji awaoneaye maskini, Ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza chakula. Wao waiachao sheria huwasifu waovu; Bali wao waishikao hushindana nao. Watu waovu hawaelewi na haki; Bali wamtafutao BWANA huelewa na zote. Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotovu wa njia angawa ni tajiri.

Soma Mithali 28