Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hesabu 11:1-3

Hesabu 11:1-3 SRUV

Kisha hao watu walikuwa kama wanung'unikao, wakinena maovu masikioni mwa BWANA; BWANA aliposikia hayo, hasira zake zikawaka; na moto wa BWANA ukawaka kati yao, ukateketeza hadi viunga vya kambi. Ndipo watu wakamlilia Musa; naye Musa akamwomba BWANA, na ule moto ukakoma. Jina la mahali hapo likaitwa Tabera kwa sababu huo moto wa BWANA ukawaka kati yao.

Soma Hesabu 11