Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 127

127
Zaburi 127
Bila Mungu, kazi ya mwanadamu haifai
Wimbo wa kwenda juu. Wa Sulemani.
1 Bwana asipoijenga nyumba,
wajengao hufanya kazi bure.
Bwana asipoulinda mji,
walinzi wakesha bure.
2Mnajisumbua bure kuamka mapema
na kuchelewa kulala,
mkitaabikia chakula:
kwa maana yeye huwapa usingizi wapendwa wake.
3Watoto ni urithi unaotoka kwa Bwana,
uzao ni zawadi kutoka kwake.
4Kama mishale mikononi mwa shujaa
ndivyo walivyo wana awazaao mtu katika ujana wake.
5Heri mtu ambaye podo lake
limejazwa nao.
Hawataaibishwa wanaposhindana
na adui zao langoni.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 127: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia