Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 128

128
Zaburi 128
Thawabu ya kumtii Bwana
Wimbo wa kwenda juu.
1Heri wale wote wamchao Bwana,
wanaoenda katika njia zake.
2Utakula matunda ya kazi yako;
baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao
ndani ya nyumba yako;
wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni
kuizunguka meza yako.
4Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa
mtu amchaye Bwana.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni
siku zote za maisha yako,
na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako.
Amani iwe juu ya Israeli.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 128: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia