Zaburi 128
128
Zaburi 128
Thawabu ya kumtii Bwana
Wimbo wa kwenda juu.
1Heri wale wote wamchao Bwana,
wanaoenda katika njia zake.
2Utakula matunda ya kazi yako;
baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao
ndani ya nyumba yako;
wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni
kuizunguka meza yako.
4Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa
mtu amchaye Bwana.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni
siku zote za maisha yako,
na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako.
Amani iwe juu ya Israeli.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 128: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.