YouVersion Logo
Search Icon

Mathayo 11:25, 26, 27, 28, 29

Mathayo 11:25 NENO

Wakati huo Yesu alisema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo.

Mathayo 11:26 NENO

Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.

Mathayo 11:27 NENO

“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: Hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.

Mathayo 11:28 NENO

“Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

Mathayo 11:29 NENO

Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha katika nafsi zenu.

Free Reading Plans and Devotionals related to Mathayo 11:25, 26, 27, 28, 29