BibleProject | Hekima ya MithaliSample

Sura ya 3: Ya Thamani kuliko Vito
Katika sura hii baba anamzungumzia tena mwanawe mara mbili, na lipo shairi kumhusu Binti Hekima.
Baba Anamzungumzia Mwanawe Mara ya Tatu
Mstari wa 1-12: Hotuba hii ni nzito na inajumuisha vifungu maarufu. Baba anaacha sisitizo la hapo awali kuhusu kuenea kwa maovu na anamhimiza mwanawe kushughulikia tabia yake mwenyewe. Chunguza matumizi ya maneno na jinsi baba anarudia neno "wewe/yako" kuonyesha matendo binafsi ya imani na matokeo yake.
Mpe Mungu kilicho bora zaidi ("Mazao yako ya kwanza") na utakuwa na utele ("maghala yako yatajaa na kufurika") Mistari miwili ya mwisho katika sehemu hii (11-12) ni tofauti kwa kuwa haiangazii manufaa ya kumheshimu Mungu. Badala yake, baba anamhimiza mwanawe kukubali nidhamu ya Mungu. Usiwe na uchungu mambo yakiwa magumu, anasema, ila amini kuwa Mungu huwakosoa Anaowapenda—kama baba kumwadhibu mwanawe.
Binti Hekima Anazungumza Mara ya Pili
Mstari wa 13-20: Hili ni shairi nzuri kuhusu hekima, na linamtumia tena mwanamke kama mhusika. "Ni wa thamani kuliko marijani; mwandishi anasema, "hakuna unachotamani kinachoweza kulinganishwa naye." Mshairi anamfafanua Binti Hekima kama mahali pa tulivu, mahali pa kupumzika na kiini cha amani—chenye uwezo. Analinganishwa na "mti wa uzima" kwenye kitabu cha Mwanzo 2:9, na katika mstari wa 19-20 tunaambiwa kuwa Mungu mwenyewe alitumia hekima kuumba ulimwengu: "Kwa hekima Mungu Aliiweka misingi ya dunia." Hekima ya Mungu ina uwezo mkuu katika ulimwengu huu na tunaweza kuipata!
Baba Anazungumza na Mwanawe Mara ya Nne
Mstari wa 21-35: Sura hii inaishia na hotuba nyingine kutoka kwa baba, akisisitiza tena kuwa njia ya hekima ni njia ya amani. Ukiwa mwenye hekima, utalala vyema, utaishi bila hofu na utajiepusha na mitego ambayo watu wengine huingia kwa urahisi. Baba anatoa ushauri kuhusu uhusiano unaolenga kuleta amani: lipa unachodaiwa, usiwadhuru watu, usiwashtaki watu bila ushahidi, na usitamani mali ambayo watu wanapata kupitia ukatili.
Scripture
About this Plan

Kitabu cha Mithali kinasema kuwa hekima ya Mungu imedhihirishwa kupitia ulimwengu na unaalikwa kushiriki. Je, ni lipi chaguo la busara kuhusiana na pesa, kazi, uhusiano na shughuli za kimaisha za kila siku? Mwongozo huu wa siku 32 utakuwezesha kusoma kitabu cha Mithali hatua kwa hatua na kufahamu mwelekeo unaopaswa kuchukua.
More
Related Plans

1 Corinthians

Unstoppable

01 - LORD'S PRAYER: Meditations by W. Phillip Keller

Financial Discipleship – the Bible on Cosigning

THE UPSIDE-DOWN KINGDOM: A 7 - Day Disovery of How God's Patterns for Living Turn Our Lives the Right Way Up by Youth Alive Aus

Sporting Life - God in 60 Seconds

Walk With God: 3 Days of Pilgrimage

Chosen for Love: A Journey With Jesus

A Heart After God: Living From the Inside Out
