Soma Biblia Kila Siku Mei 2021Sample

Wakajikwaa kwake (m.3). Yesu alikuwa amefika nyumbani Nazareti (ni maana ya “nchi ya kwao” katika m.1). Watu wa nyumbani walikuwa wanashangaa. Kwa upande mmoja walikubali kuwa mafundisho yake na matendo yake ni ya pekee sana, maana waliposikia [aliyowafundisha] wakashangaa, wakisema, Huyu ameyapata wapi haya? Na, Ni hekima gani hii aliyopewa huyu? Na, Ni nini miujiza hii mikubwa inayotendeka kwa mikono yake? (m.2). Kwa upande mwingine walijua Yesu ni seremala tu wala si mwalimu wa dini (mwanatheolojia) aliyepitia mafunzo kwa walimu wao wa dini ya Kiyahudi (m.3). Huenda walifikiri anayafanya kwa nguvu ya Shetani? Ugumu wao wa kupokea ulimfanya Yesu kuwaambia, Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamaa zake, na nyumbani mwake. Neno hili la Yesu katika m.4 lituonye kwamba tusijikwae, Mungu akiamua kumjalia mtu wa kwetu kwa njia ya pekee!
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ayubu. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

Ruth | Chapter Summaries + Study Questions

Stormproof

Let Us Pray

Unapologetically Sold Out: 7 Days of Prayers for Millennials to Live Whole-Heartedly Committed to Jesus Christ

Breath & Blueprint: Your Creative Awakening

The Lies We Believe: Beyond Quick Fixes to Real Freedom Part 2

Faith in Hard Times

FruitFULL - Faithfulness, Gentleness, and Self-Control - the Mature Expression of Faith

Homesick for Heaven
