INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA TISASample

YESU AMPONYA MWANAMKE ALIYEJIKUNYATA
"Basi Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo siku ya Sabato.Wakati uo huo akaja mwanamke mmoja aliyekuwa na pepo mchafu, naye alikuwa amepinda mgongo kwa muda wa miaka kumi na minane, wala alikuwa hawezi kunyoka wima."
Yesu alipomwona, akamwita akamwambia, “Mwanamke, uwe huru, umepona ugonjwa wako.”
Yesu alipomwekea mikono yake, mara akasimama wima akaanza kumtukuza Mungu.
Lakini mkuu wa sinagogi, akakasirika kwa sababu Yesu alikuwa ameponya mtu siku ya Sabato. Kwa hiyo mkuu wa sinagogi akaendelea kuuambia ule umati wa watu,
“Kuna siku sita ambazo watu wanapaswa kufanya kazi, katika siku hizo, njoni mponywe, lakini si kuja kuponywa siku ya Sabato.”
Lakini Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Je, kila mmoja wenu hamfungulii ng'ombe wake au punda wake kutoka zizini akampeleka kumnywesha maji siku ya Sabato?
Je, huyu mwanamke, ambaye ni binti wa Abrahamu, aliyeteswa na Shetani akiwa amemfunga kwa miaka yote hii kumi na minane, hakustahili kufunguliwa kutoka katika kifungo hicho siku ya Sabato?”
Aliposema haya, wapinzani wake wakaaibika, lakini watu wakafurahi kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyoyafanya.
Scripture
About this Plan

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana
More
Related Plans

How to Pray for Missionaries

Rebellion Meets Grace — the Story of the Prophet Jonah

Biblical Success - Crossing the Finish Line. Our Race Won, What’s Heaven Like?

Holy Spirit - Breath of God

Journey Through Revelation

Boundaries: A Biblical Perspective

Dear Black Woman, You Are Not Alone in Your Grief

Cherished & Chosen: A 7-Day Challenge for Single Women

Relentless Love: Reflections on the Book of Jonah
