Injili Ulimwenguni - Sehemu 1Sample

Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta. Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa Sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa na majibu aliyoyatoa. Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamwuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?” Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtii kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
Scripture
About this Plan

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana.
More
Related Plans

After Your Heart

Overcoming Offense

Journey Through Psalms & Song of Songs

Back to School, Back to You

BibleProject | Redemption in the Biblical Story

Always Abounding: A 3-Day Devotional on Hope and Faith

Forever Open: A Pilgrimage of the Heart

Journey Through Esther, Ezra & Nehemiah

God of the in Between
