1
Yakobo 1:2-3
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Wandugu zangu, muhesabu kuwa ni jambo la furaha sana wakati munapopata majaribu ya namna mbalimbali, kwa maana munajua kwamba kupimwa kwa imani yenu kunawaletea uvumilivu.
तुलना
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:2-3
2
Yakobo 1:5
Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:5
3
Yakobo 1:19
Wandugu zangu wapendwa, mukumbuke neno hili: kila mutu anapaswa kuwa mwepesi kwa kusikia, lakini asikuwe mwepesi kwa kusema na kukasirika.
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:19
4
Yakobo 1:4
Lakini sherti uvumilivu ule utimize kazi yake, kusudi mupate kuwa wakamilifu na watimilifu wasiopungukiwa na kitu.
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:4
5
Yakobo 1:22
Musijidanganye ninyi wenyewe kwa kusikiliza tu neno la Mungu, lakini mulitimize kwa matendo.
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:22
6
Yakobo 1:12
Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:12
7
Yakobo 1:17
Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:17
8
Yakobo 1:23-24
Kwa maana mutu anayesikia neno tu pasipo kulitimiza, anafanana na mutu anayejiangalia sura yake mwenyewe katika kioo. Kisha kujiangalia, anajiendea, na mara moja anasahau namna anavyokuwa.
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:23-24
9
Yakobo 1:27
Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:27
10
Yakobo 1:13-14
Wakati mutu anapojaribiwa, asiseme hivi: “Ninajaribiwa na Mungu!” Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na ubaya, wala yeye mwenyewe hawezi kumujaribu mutu. Lakini kila mutu anajaribiwa wakati anapovutwa na kudanganywa na tamaa yake mbaya mwenyewe.
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:13-14
11
Yakobo 1:9
Ndugu anayekuwa masikini afurahi kwa sababu Mungu anamupandisha
अन्वेषण गर्नुहोस् Yakobo 1:9