YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 53

53
Mtu asiyemcha Mungu
(taz Zaburi ya 14)
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Mahalathi. Utenzi wa Daudi)
1 # Rom 3:10-12 Wapumbavu hujisemea moyoni:
“Hakuna Mungu!”
Wote wamepotoka kabisa,
wametenda mambo ya kuchukiza;
hakuna hata mmoja atendaye jema.
2Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni,
aone kama kuna yeyote mwenye busara,
kama kuna yeyote anayemtafuta Mungu.
3Lakini wote wamekosa,
wote wamepotoka pamoja,
hakuna atendaye mema,
hakuna hata mmoja.
4“Je, hao watendao maovu hawana akili?
Wanawatafuna watu wangu kama mikate;
wala hawanijali mimi Mungu!”
5Hapo watashikwa na hofu kubwa,
hofu ambayo hawajapata kuiona;
maana Mungu ataitawanya mifupa ya adui,
hao wataaibika maana Mungu amewakataa.
6Laiti ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Siyoni!
Mungu atakaporekebisha hali ya watu wake,
wazawa wa Yakobo watashangilia;
Waisraeli watafurahi.

Currently Selected:

Zaburi 53: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy