YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 28

28
Kuomba msaada
(Zaburi ya Daudi)
1Nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu!
Ewe mwamba wa usalama wangu usiniwie kama kiziwi,
la sivyo kama usiponisikiliza,
nitakuwa kama wale washukao shimoni kwa wafu.
2Sikiliza sauti ya ombi langu,
ninapokulilia unisaidie,
ninapoinua mikono yangu kuelekea maskani yako takatifu.
3Usinipatilize pamoja na watu wabaya,
pamoja na watu watendao maovu:
Watu wasemao na wenzao maneno ya amani,
kumbe wamejaa uhasama moyoni.
4 # Taz Ufu 22:12 Uwaadhibu kadiri ya matendo yao,
kufuatana na maovu waliyotenda.
Waadhibu kadiri ya matendo yao wenyewe;
uwatendee yale wanayostahili.
5Hawajali matendo ya Mwenyezi-Mungu;
hawatambui mambo aliyoyafanya.
Kwa sababu hiyo atawabomoa,
wala hatawajenga tena upya.
6Atukuzwe Mwenyezi-Mungu,
maana amesikiliza ombi langu.
7Mwenyezi-Mungu ndiye nguvu yangu na ngao yangu;
tegemeo la moyo wangu limo kwake.
Amenisaidia nami nikashangilia kwa moyo;
kwa wimbo wangu ninamshukuru.
8Mwenyezi-Mungu ni nguvu ya watu wake;
yeye ni kimbilio la wokovu kwa mfalme wake mteule.
9Ee Mungu, uwaokoe watu wako;
uwabariki watu hao walio mali yako.
Uwe mchungaji wao na kuwategemeza milele.

Currently Selected:

Zaburi 28: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy