Zaburi 150
150
Zaburi ya kumsifu Mungu
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Msifuni Mungu katika patakatifu pake;
msifuni katika mbingu zake kuu.
2Msifuni kwa sababu ya matendo yake makuu;
msifuni kwa ajili ya utukufu wake mkuu.
3Msifuni kwa mlio wa tarumbeta;
msifuni kwa zeze na kinubi!
4Msifuni kwa ngoma na kucheza;
msifuni kwa filimbi na banjo!
5Msifuni kwa kupiga matoazi.
Msifuni kwa matoazi ya sauti kubwa.
6Kila kiumbe hai kimsifu Mwenyezi-Mungu!
Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Currently Selected:
Zaburi 150: BHN
Highlight
Share
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.