YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 149

149
Wimbo wa ushindi
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Mwimbieni Mwenyezi-Mungu wimbo mpya;
msifuni katika kusanyiko la waaminifu!
2Furahi ee Israeli kwa sababu ya Muumba wako,
wakazi wa Siyoni shangilieni kwa sababu ya Mfalme wenu.
3Lisifuni jina lake kwa ngoma,
mwimbieni kwa ngoma na zeze.
4Maana Mwenyezi-Mungu hupendezwa na watu wake;
yeye huwapamba wanyonge kwa ushindi.
5Watu waaminifu wafurahi kwa fahari;
washangilie hata walalapo.
6Wabubujike sifa kuu za Mungu,
na panga zenye makali kuwili mikononi mwao,
7wawalipe kisasi watu wa mataifa,
wawaadhibu watu wasiomjua Mungu;
8wawafunge wafalme wao kwa minyororo,
na viongozi wao kwa pingu za chuma,
9kusudi watekeleze adhabu iliyoamriwa!
Hiyo ndiyo fahari ya waaminifu wa Mungu.
Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Currently Selected:

Zaburi 149: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy