YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 148

148
Ulimwengu wote umsifu Mungu
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Msifuni Mwenyezi-Mungu kutoka mbinguni,
msifuni kutoka huko juu mbinguni.
2Msifuni, enyi malaika wake wote,
msifuni, enyi majeshi yake yote.
3Msifuni, enyi jua na mwezi,
msifuni, enyi nyota zote zingaazo.
4Msifuni, enyi mbingu za juu,
na maji yaliyo juu ya mbingu.
5Vyote vilisifu jina la Mwenyezi-Mungu,
maana yeye aliamuru, na vyote vikawa.
6Yeye aliviweka mahali pao daima,
kwa amri ambayo haiwezi kubatilishwa.
7Msifuni Mwenyezi-Mungu kutoka duniani;
enyi majoka ya baharini na vilindini, msifuni.
8Msifuni enyi moto, mvua ya mawe na theluji,
upepo wa tufani unaotimiza amri yake!
9Msifuni enyi milima na vilima,
miti ya matunda na misitu!
10Msifuni enyi wanyama wa porini na wafugwao,
viumbe vitambaavyo na ndege wote!
11Msifuni enyi wafalme na mataifa yote;
viongozi na watawala wote duniani!
12Msifuni enyi wavulana na wasichana;
wazee wote na watoto pia!
13Nyote lisifuni jina la Mwenyezi-Mungu,
maana jina lake peke yake latukuka;
utukufu wake wapita dunia na mbingu.
14Amewapa watu wake nguvu;
heshima kwa watu wote waaminifu,
watu wa Israeli wapenzi wake.
Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Currently Selected:

Zaburi 148: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy