YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 127

127
Bila Mungu kazi ya binadamu haifai
(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Solomoni)
1Mwenyezi-Mungu asipoijenga nyumba,
waijengao wanajisumbua bure.
Mwenyezi-Mungu asipoulinda mji,
waulindao wanakesha bure.
2Mnajisumbua bure kuamka mapema asubuhi
na kuchelewa kwenda kupumzika jioni,
mjipatie chakula kwa jasho lenu.
Mungu huwaruzuku walio wake hata walalapo.
3Watoto ni riziki kutoka kwa Mwenyezi-Mungu;
watoto ni tuzo lake kwetu sisi.
4Watoto waliozaliwa wazazi wakiwa bado vijana,
ni kama mishale mikononi mwa askari.
5Heri mtu aliye na mishale hiyo kwa wingi.
Hatashindwa atakapokabiliana na adui mahakamani.

Currently Selected:

Zaburi 127: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy