YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 109

109
Lalamiko la mtu taabuni
(Kwa Mwimbishaji. Wimbo wa Daudi)
1Usinyamaze, ee Mungu ninayekusifu!
2Watu waovu na wadanganyifu wanishambulia,
wanasema uongo dhidi yangu.
3Wanasema maovu juu yangu,
na kunishambulia bila kisa.
4Ingawa niliwapenda, walinishtaki,
hata hivyo niliwaombea dua.
5Wananilipa uovu kwa wema wangu,
na chuki kwa mapendo yangu.
6Umweke hakimu mbaya dhidi ya adui yangu;
na mshtaki wake ampeleke mahakamani.
7Anapohukumiwa apatikane na hatia;
lalamiko lake lihesabiwe kuwa kosa jingine.
8 # Taz Mate 1:20 Siku za maisha yake ziwe chache,
mtu mwingine na achukue kazi yake!
9Watoto wake wawe yatima,
na mke wake awe mjane!
10Watoto wake watangetange na kuombaomba;
wafukuzwe katika magofu ya nyumba zao!
11Anayemdai kitu amnyanganye mali yake yote;
na wageni wanyakue mapato ya jasho lake!
12Pasiwe na mtu wa kumwonea huruma,
au Kuwatunza watoto wake yatima!
13Wazawa wake wote wafe;
jina lake lisahauliwe katika kizazi kijacho!
14Mwenyezi-Mungu aukumbuke uovu wa wazee wake,
dhambi za mama yake zisifutwe kamwe!
15Mwenyezi-Mungu azikumbuke dhambi zao daima;
lakini wao wenyewe wasahauliwe duniani.
16Mwovu huyo hakujali kabisa kuwa na huruma,
ila aliwadhulumu maskini na fukara,
kadhalika na watu wanyonge mpaka kifo.
17Yeye alipenda kulaani watu,
laana na impate yeye mwenyewe.
Hakuwatakia wengine baraka,
basi, asipate baraka yeye mwenyewe.
18Kwake kulaani ni kama kuvaa nguo,
basi, laana hizo zimloweshe kama maji,
zimwingie mifupani mwake kama mafuta.
19Laana zimfunike kama nguo,
zimzunguke daima kama ukanda.
20Mwenyezi-Mungu awalipe hayo hao watu wanaonishtaki,
naam hao wanaosema mabaya dhidi yangu.
21Lakini ee Mwenyezi-Mungu, Bwana wangu,
unitendee kadiri ya hisani yako;
uniokoe, kwa sababu ya wema wa fadhili zako!
22Mimi ni maskini na fukara;
nimejeruhiwa mpaka moyoni mwangu.
23Natoweka kama kivuli cha jioni;
nimepeperushwa kama nzige.
24Magoti yangu yamenyongonyea kwa mfungo;
nimebaki mifupa na ngozi.
25 # Taz Mat 27:39; Marko 15:29 Nimekuwa dhihaka tupu kwa watu;
wanionapo hutikisa vichwa vyao kwa dharau.
26Unisaidie, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu;
uniokoe kadiri ya fadhili zako.
27Waoneshe watu kuwa ndiwe uliyetenda hayo,
wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ndiwe uliyefanya hivyo.
28Waache walaani, lakini wewe unibariki;
wanaonishambulia waaibike, nami mtumishi wako nifurahi.
29Maadui zangu na wavishwe fedheha;
wajifunike aibu yao kama blanketi.
30Nitamshukuru sana Mwenyezi-Mungu kwa sauti;
nitamsifu kati ya kundi kubwa la watu,
31kwa maana yeye humtetea maskini,
humwokoa wakati anapohukumiwa.

Currently Selected:

Zaburi 109: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy