YouVersion Logo
Search Icon

Methali 19

19
1Afadhali maskini aishiye kwa unyofu,
kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu.
2Haifai mtu kuwa bila akili;
mwenda harakaharaka hujikwaa.
3Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake,
huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.
4Mali huvuta marafiki wengi wapya,
lakini maskini huachwa bila rafiki.
5Shahidi mwongo hataacha kuadhibiwa;
asemaye uongo hataepa adhabu.
6Watu wengi hujipendekeza kwa wakuu;
kila mtu hutaka kuwa rafiki ya mtu mkarimu.
7Maskini huchukiwa na ndugu zake;
marafiki zake ndio zaidi: Humkimbia!
Hata awabembeleze namna gani hatawapata.#19:7 Hata … hatawapata: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
8Ajipatiaye hekima anaipenda nafsi yake;
anayezingatia busara atastawi.
9Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa;
asemaye uongo ataangamia.
10Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa,
tena ni vibaya zaidi mtumwa kuwatawala wakuu.
11Mwenye busara hakasiriki upesi;
kusamehe makosa ni fahari kwake.
12Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba,
lakini wema wake ni kama umande juu ya majani.
13Mtoto mpumbavu ni balaa kwa baba yake;
na ugomvi wa mke ni kama matone ya mvua yasiyoisha.
14Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa wazee wake,
lakini mke mwenye busara hutoka kwa Mwenyezi-Mungu.
15Uzembe ni kama usingizi mzito;
mtu mvivu atateseka kwa njaa.
16Anayeshika amri anasalimisha maisha yake;
anayepuuza agizo atakufa.
17Anayemsaidia maskini anamkopesha Mwenyezi-Mungu;
Mwenyezi-Mungu atamlipa kwa tendo lake jema.
18Mrudi mwanao kungali bado na tumaini,
lakini usimwadhibu kiasi cha kumwangamiza.
19Mtu wa hasira kali lazima apate adhabu;
ukimwachia mara moja itakubidi kumwachia tena.#19:19 ukimwachia … tena: Au ukimtoa kwenye matatizo hali yake huwa mbaya zaidi.
20Sikiliza shauri na kupokea mafundisho,
upate hekima ya kukufaa siku zijazo.
21Kichwani mwa mtu mna mipango mingi,
lakini anachokusudia Mwenyezi-Mungu ndicho kitakachofanyika.
22Kinachotakiwa kwa mtu ni uaminifu;
afadhali mtu maskini kuliko mtu mwongo.
23Kumcha Mwenyezi-Mungu kunaleta uhai;
amchaye hujaliwa pumziko la kutosheleza,
wala hatapatwa na baa lolote.
24Mvivu ni kama mtu atiaye mkono katika sahani ya chakula,
lakini hana nguvu ya kuuinua hadi mdomoni.
25Mwadhibu mwenye mzaha naye mjinga atapata akili;
mwonye mwenye busara naye atapata maarifa.
26Anayemdhulumu baba yake na kumfukuza mama yake,
ni mtoto asiyefaa na mpotovu.
27Mwanangu, ukiacha kusikiliza mafundisho,
utapotea mara mbali na maneno ya hekima.
28Shahidi asiyefaa kitu huidhihaki haki;
na kinywa cha mwovu hubugia uovu.
29Adhabu iko tayari kwa wenye mzaha,
mijeledi imetayarishwa kuchapa migongo ya wapumbavu.

Currently Selected:

Methali 19: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy