Malaki 4
4
Siku ya Mwenyezi-Mungu inakuja
1Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema: “Tazama, siku yaja, nayo inawaka kama tanuri. Wenye kiburi na waovu wote watatupwa humo na kuteketea kama mabua makavu; watateketea kabisa pasibaki hata alama. 2Lakini kwa ajili yenu nyinyi mnaonicha, uwezo wangu wa kuokoa utawachomozea kama jua lililo na nguvu za kuponya kwenye mionzi yake. Mtatoka mkirukaruka kama ndama watokapo zizini mwao. 3Siku hiyo mtawakanyagakanyaga waovu, nao watakuwa kama majivu chini ya nyayo zenu. Nasema mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
4“Kumbukeni sheria, kanuni na maagizo yangu niliyomwamuru Mose mtumishi wangu kule mlimani Horebu, ili awaamuru watu wote wa Israeli.
5 # Taz Mat 11:14; 17:10-13; Marko 9:11-13; Luka 1:17; Yoh 1:21 “Tazama, kabla ya kufika siku ile kuu na ya kutisha, nitamtuma nabii Elia. 6Nabii Elia atawapatanisha wazazi na watoto wao; la sivyo, nitakuja na kuiangamiza nchi yenu.”
Currently Selected:
Malaki 4: BHN
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Malachi 4
4
The Great Day of God
1“For behold, #Ps. 21:9; (Nah. 1:5, 6; Mal. 3:2, 3; 2 Pet. 3:7)the day is coming,
Burning like an oven,
And all #Mal. 3:18the proud, yes, all who do wickedly will be #Is. 5:24; Obad. 18stubble.
And the day which is coming shall burn them up,”
Says the Lord of hosts,
“That will #Amos 2:9leave them neither root nor branch.
2But to you who #Mal. 3:16fear My name
The #Matt. 4:16; Luke 1:78; Acts 10:43; 2 Cor. 4:6; Eph. 5:14Sun of Righteousness shall arise
With healing in His wings;
And you shall go out
And grow fat like stall-fed calves.
3#Mic. 7:10You shall trample the wicked,
For they shall be ashes under the soles of your feet
On the day that I do this,”
Says the Lord of hosts.
4“Remember the #Ex. 20:3Law of Moses, My servant,
Which I commanded him in Horeb for all Israel,
With #Deut. 4:10the statutes and judgments.
5Behold, I will send you #(Matt. 11:14; 17:10–13; Mark 9:11–13; Luke 1:17); John 1:21Elijah the prophet
#Joel 2:31Before the coming of the great and dreadful day of the Lord.
6And he will turn
The hearts of the fathers to the children,
And the hearts of the children to their fathers,
Lest I come and #Zech. 14:12strike the earth with #Zech. 5:3a curse.”
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
The Holy Bible, New King James Version, Copyright © 1982 Thomas Nelson. All rights reserved.